Je! Tuwabatize Watoto Wachanga?
Na: Larry Ritter
Watu wengine katika dini zao wana kawaida ya kubatiza watoto wadogo. Lakini Biblia inasemaje kuhusu hilo? Je! Hivyo ndivyo Mungu apendavyo? Je! Yesu alifundisha lolote kuhusu lilo? Je! Upo mfano wowote katika Biblia ambapo mtoto alibatizwa?
Kama kawaida tunapaswa kupata maelekezo na mifano kutoka kwenye maneno ya Mungu Biblia (2 Tim. 3:16-17), “Kila andiko lenye pumzi ya Mungu lafaa kwa mafundisho na kwa kuaonya watu makosa yao na kuwaongoza na kuwaadabisha katika haki ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda haki.”Biblia ndio nguvu yetu na mamlaka ya mwisho katika mambo yote ya kiroho. Tuangalie na tuone Mungu anasemaje kuhusu ubatizo.
1.Warumi 10:17, Paulo anasema, “Imani huja kwa kusikia na kusikia huja kwa neno la Mungu.” Je! Mtoto mchanga anaweza kusikia neno la Mungu kwa kufundishwa na akakubali kwa kumwamini Mungu?
2. Marko 16:15, 16, Yesu anasema, “Nendeni ulimwenguni kote mkahubiri injili kwa kila kiumbe, atakayeamini na kubatizwa ataokolewa, asiyeamini atahukumiwa.” Je! Mtoto mchanga aweza kuamini? Je! Wanao uwezo wa kusikia injili, kufikili hilo na wakaamini?
3. Matendo 2:38, Hapa Petro alikuwa akiwaambila watu waliosikia na wakachomwa mioyo yao na walipouliza tufanye nini Petro aliwaambia, “Tubuni mkabatizwe katika jina la Yesu Kristo kwa ondoleo la dhambi.” Je! Vitoto vichanga vinaweza kutubu, au kubadili njia zao? Kama ndivyo wata tubu nini? Ama ubatizo ni nini? Petro anasema hapa kwa ondoleo la dhambi. Je! Watoto wanayo dhambi inayohitaji kuondolewa? Hapana, watoto wadogo hawana dhambi, watoto wanafahamu jema na baya? Hapana.
4. Matendo 8:12, “Na walipoamini Filipo akahubiri mambo ya husuyo ufalme wa Mungu na jina la Yesu Kristo, wakabatizwa nao wana wake na wanaume.” Tena hapa watoto waweza kuamini walichohubiliwa?
5. Matendo 8:36-37, Hapa Filipo alikuwa akimhubiria mtu mmoja kuhusu Yesu wakafika penye maji naye akasema, “Maji si haya, ni nini kitakochonizuia nisibatizwe? Naye Filipo akasema, ukiamini kwa moyo wote inawezekana, naye akajibu akasema, Naamini kuwa Yesu Kristo ni Mwana wa Mungu.” Kabla ya mtu kubatizwa anapaswa kuamini kwa moyo wake wote. Je! Mtoto mchanga aweza kufanya hivyo?
6. Matendo 16:30-34, Mlinzi wa geleza alipotaka kujua afanya nini ili aokolewe Paulo na Silasi walimwambia, “Mwamini Bwana Yesu Kristo nawe utaokoka na nyumba yako.” Hapa walikuwa na maana ya kwamba nyumba yote ingeokoka kwa imani ya yule mlinzi? Angalia neno linaongelewa kwa wote waliokuwamo kwenye nyumba, inasema “yeye na wote wakabatizwa” wakati huo huo. Je! Inasema yeye alikuwa na watoto wachanga? Kwa hiyo tuamini alikuwa na watoto wachanga wakati Biblia haisemi?
7. Mathayo 18:1-5, Watu wengine wanachukua kipengele hiki kama mamlaka ya kuwabatiza watoto. Kwanza kabisa ubatizo haujatajwa popote hapa katika kifungu hiki cha maandiko. Wala haikuwahi kufikiliwa. Pia isingewezekana wabatizwe katika mauti (Rum. 6:3-5) hata hivyo katika swala hilo hata Yesu mwenyewe alikuwa bado hajafa.
Lakini kwa nini Yesu alifanya hivyo ni kwamba wanafunzi wake waaje kujilinganisha kuwa ni yupi mkubwa kati yao, walihitaji kunyenyekea kama mtoto mdogo. Utu wa mtoto ndio unaongelewa hapa. Huyo mtoto hakubatizwa.
Kwa kuhitimisha ni kwamba ubatizo sio kwa watoto. Ubatizo sio kwao ambao hawajakuwa bado kufahamu mema na mabaya. Ubatizo ni kwa wale tu walitenda dhambi na wanahitaji ondoleo la dhambi. Wachanga hawana dhambi, hawajitambui wenyewe, hawawezi kuamini. Kama hawaamini, kwa nini wabatizwe? Kama watoto hawaamini kabla ya kubatizwa kwa nini mtu mwingine afanye badala yao? Kwa nini wanafaunzi wa kwanza walifundisha nyumba kwa nyumba (Mdo. 20:20) kama kuamini sio muhimu? Je! Itakuwaje endapo mtu mzima akikataa kubatizwa? Utambatiza tu hata japo yeye hataki? Inakuaje sasa kwa watoto ambao hata hawajui kinachoendelea. Watoto hawahitaji kubatizwa.
KANISA LA KRISTO