Tags

, ,

I. UBATIZO WA MAJI UMEAMRIWA.

a. Mt. 28:19, “Basi, enendeni mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi wangu mkiwabatiza kwa jina la Baba na Mwana na Roho Mtakatifu.”

b. Mdo. 2:38, “Petro akawaambia, tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu….”

c. Mdo 10:48, “Akaamuru wabatizwe kwa jina lake Yesu Kristo.”

d. Mdo. 18:8, “..na Wakorintho wengi waliposikia, waliamini, wakabatizwa.”

e. Mdo. 22:16, “Basi, sasa unakawilia nini? Simama ubatizwe ukaoshwe dhambi zako..”

f. Rum. 6:3, “Hamfahamu ya kuwa sisi sote tuliobatizwa katika kristo yesu tulibatizwa katika mauti yake.”

g. Hapa tumekwisha kuona jinsi Kristo na mitume walivyoamuru ubatizo kama ni kanuni ya wokovu (au ondoleo la dhambi) na kwa kuongozwa na Kristo.

II. NI AKINA NANI WANAOHUSIKA KUBATIZWA?

a. Ni wale wanaoweza kufundishwa, Mt. 28:18-20.

b. Ni wale wanaoamini, Mk. 16:15-16.

c. Ni wale waliotubu, Mdo. 2:38.

d. Ni wale waliomkiri, Mdo. 8:37. “Filipo akasema, ukiamini kwa moyo wako wote, inawezekana akajibu, akanena, naamini ya kwamba Yesu Kristo ndiye Mwana wa Mungu.”

e. Watoto wadogo sio somo la ubatizo.  Hawajapotea; mtu hawezi kuokolewa kama hajapotea. Watoto wadogo hawajapotea wako salama hawana dhambi, Eze.18:20.  Pia, Watoto wadogo hawawezi kuamini, kutubu, au kumkiri Kristo, Mdo. 2:37.

III. WENGINE WALIBATIZWA TENA KATIKA AGANO JIPYA?

a. Paulo aliwakuta watu waliobatizwa ubatizo wa Yohana kabla ya sheria za Kristo kukamilika, Mdo. 19:3.

b. Kwa mafundisho ya Paulo, waliona inawalazimu kubatizwa tena kwa jina la Bwana Yesu; na kwa madhumuni aliyoyaeleza Kristo.

c. Wengi siku hizi wamebatizwa kwa njia isiyo sawa au kwa madhumuni yasiyo sawa; hawa wanapaswa kubatizwa kwa ondoleo la dhambi, Mdo. 2:38; Rum. 6:1-11.

IV. KUNYUNYIZIA, KUMWAGIA AU KUZAMISHA NI UPI?

a. Ubatizo ni kuzika: “Mkazikwa pamoja naye katika ubatizo; na katika huo mkafufuliwa pamoja naye, kwa kuziamini nguvu za Mungu aliyemfufua katika wafu,” Kol. 2:12.

b. Ubatizo unahitajika. 1) Maji mengi, Yoh. 3:23. 2) Ni kutelemka majini, Mdo. 8:38. 3) Ni kuzama ndani ya maji, Mdo. 8:38. 4) Ni kupanda toka majini, Mt. 3:16. Yesu alibatizwa (kuzamishwa) na Yohana, si kwa ondoleo la dhambi, lakini ni kwa kuitimiza haki yote. Kwani Yeye hakuwa na dhambi.

c. Katika neno la Mungu “Ubatizo.”  1) “Ubatizo” tafsiri ya Kiyunani katika Agano Jipya ni baptizo. Neno hili linaeleza maana yake ni kutumbukiza, ni kuzamisha, na kadhalika.” 2) “Kunyunyiza” tafsiri ya Kiyunani katika Agano Jipya ni “Rantizo;” na kumwagia ni “Cheo”. 3) Mahali popote ambapo neno “ubatizo” linaonekana au kusemwa au kuandikwa ni baptizo sio rantizo au cheo.

V. Historia ya Affusio kunyunyizia au kumwagia (Kanisa lilianza mwaka 33 B.K.).

a. Mageuzi haya yaliandikwa mnamo 251 B.K. alipokuwa amelala kitandani kwa ajili ya ugonjwa.

b. Hapo kwanza, Affusio ilikuwa ikubaliwe na watawala kwa udhaifu.

c. Baraza la Ravenna, wakati wa 1311 B.K. liliutambua ubatizo wa kunyunyiza katika kanisa Katoliki.

d. Affusio ni uzushi wa wanadamu, ambao hauwezi kutimiza mpango wa Mungu wa wokovu.

VI. Kusudi la Ubatizo wa Agano Jipya.

a. “Unawaokoa ninyi pia siku hizi,” 1 Pet. 3:20-21.

b. Na matokeo yake ni msamaha wa dhambi, Mdo. 2:38.

c. “Unasafisha dhambi,” Mdo. 22:16.

d. “Unatuweka ndani ya Kristo,” Gal. 3:36-27.

e. Tulibatizwa “katika mauti ya Kristo,” Rum. 6:3-4. Kristo alimwaga damu kwa mauti yake, Yoh. 19:32-37. Tulibatizwa katika mauti yake. Ni katika ubatizo unaposhiriki damu ambayo husafisha dhambi zetu.

http://www.kanisalakristo.com